Prof. Idrissa B. Mshoro
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Prof. Idrissa B. Mshoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda (TIRDO) kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia tarehe 01 aprili, 2011. Prof. Mshoro ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi wadhifa alioupata tangu mwezi Septemba, 2007 akitokea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kama Mhadhiri.
Wajumbe wengine walioteuliwa ni Bwana Bernard Mchomvu- Afisa Mtendaji Mkuu wa Millennium Challenge Account, Tanzania, Bwana Ali Rajab Mohamed -Mkurugenzi, Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Bibi Suzy Lazier- Mkurugenzi, Tanzania Food Processors Association, Bibi Eline Sikazwe- Mkurugenzi, Idara ya Maendeleo ya Viwanda pamoja na Dkt Asifa Nanyaro-Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania.
Soma Zaidi MICHUZI Blog
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Toa Maoni Yako Kwa Uhuru